IQNA

Qatar imeandaa mashindano ya Qur'ani katika Mwezi wa Ramadhani

12:55 - April 15, 2021
Habari ID: 3473815
TEHRAN (IQNA)- Taasisi ya Kijiji ya Utamaduni (Katara) nchini Qatar imetangaza harakati kadhaa za mitandaoni katika mwezi mtukufu wa Ramadhani kama vile mashindano ya Qur'ani na maonyesho.

Shughuli hizo zinafanyika mitandaoni au kwa njia ya intaneti kutokana ikiwa ni katika fremu yaa kuzuia maambukizi ya COVID-19.

Zawadi ya Katara ya Qiraa ya Qur'ani Tukufu ni mashuhuri katika ulimwengu wa wa Kiislamu ambapo washindi hutangazwa katika televisheni ya Qatar.

Taasisi ya Katar pia ina mashindano maalumu y Qur'ani Tukufu maalumu kwa watoto katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.

Mbali na mashindano ya Qur'ani Taasisi ya Katara pia huandaa mashindano ya mashairi ya Kiarabu na pia taasisi hiyo imetayarisha kipindi maarufu cha katuni ambacho kinajulikana kama Tamour na Tamoura.

474460/

captcha