IQNA

Umoja wa Waislamu

Msomi wa India: Maadui hawapendi kuona maendeleo ya Waislamu

7:19 - October 18, 2022
Habari ID: 3475947
TEHRAN (IQNA) – Mwanazuoni wa Kiislamu wa India anasema maadui wanaleta migawanyiko katika ulimwengu wa Kiislamu kwa vile hawataki kuona maendeleo ya Waislamu.

Tofauti kati ya Waislamu ni matokeo ya njama za maadui, Syed Mohammad Taqi, Imamu wa Msikiti wa Chuo Kikuu cha Aligarh Muslim, aliiambia IQNA kwa mnasaba wa Wiki ya Umoja wa Kiislamu.

Maadui wanafurahia mgawanyiko katika ulimwengu wa Kiislamu kwani hawataki kuona maendeleo ya Umma wa Kiislamu, aliongeza.

Qur'ani Tukufu inasisitiza haja ya kudumisha umoja na kuepuka mifarakano kati ya Waislamu, alibainisha.

Aliwashauri Waislamu kuzingatia mambo makubwa yanayofanana kati ya madhehebu mbalimbali, kama vile Tawhid (kuamini Mungu mmoja), Qur’ani, na Nabuwat (utume), badala ya kuzingatia tofauti ndogo ndogo.

Alitaja kuwaalika Waislamu wa madhehebu mbali mbali kwenye sherehe za kidini na kuhudhuria hafla za kitamaduni kuwa ni njia ya kujenga umoja.

Kulingana na msomi huyo, aina yoyote ya shida au tofauti inapaswa kutatuliwa kwa mazungumzo.

Siku ya 17 ya Rabi al-Awwal, iliyoangukia Oktoba 13 mwaka huu, inaaminika na Waislamu wa Shia kuwa ni siku ya kuzaliwa kwa Mtume Mohammad (SAW), huku Waislamu wa Sunni wakizingatia siku ya 12 ya mwezi (Jumapili, Oktoba 9). kama siku ya kuzaliwa nabii wa mwisho.

Muda kati ya tarehe hizo mbili huadhimishwa kila mwaka kama Wiki ya Umoja wa Kiislamu.

Wiki ya Umoja wa Kiislamu ni ubunifu wa Muasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hayati Imam Khomeini (RA) katika muongo wa 1980.

4091762

captcha