IQNA

Mashindano ya Qur'ani

Qari wa Bahrain ashinda Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani ya Malaysia

21:16 - October 25, 2022
Habari ID: 3475987
KUALA LUMPUR (IQNA) - Washindi wakuu wa Mashidano ya 62 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Malaysia walitangazwa na kutunukiwa zawad katika hafla ya kufunga hapa Jumatatu.

Sherehe hizo katika Ukumbi wa Kuala Lumpur Convention Centre (KLCC) zilihudhuriwa na viongozi wa ngazi za juu, akiwemo mfalme wa Malaysia, Sultan Abdullah Ri'ayatuddin Al-Mustafa Billh Shah, Malkia Tunku Azizah Aminah Maimunah, Waziri Mkuu Ismail Sabri Yaakob na Waziri katika Idara ya Waziri Mkuu (Mambo ya Dini) Idris Ahmad, pamoja na viongozi wa kidini, mabalozi wa nchi za Kiislamu, wajumbe wa jopo la majaji, washindani na idadi kubwa ya wananchi.

Miongoni mwa waliohudhuria ni Balozi wa Iran nchini Malaysia Ali Asghar Mohammadi, Mwambata wa Utamaduni katika Ubalozi wa Iran Mohammad Ali Oraei Karimi, na ujumbe wa Qur'ani unaoongozwa na Naibu wa Wizara ya Utamaduni na Miongozo ya Kiislamu ya Iran Ali Reza Moaf.

Bahraini Qari Wins Malaysia Int’l Quran Contest, Host Country’s Contender Comes 1st in Women’s Category

Baada ya wimbo wa taifa wa Malaysia na kusomwa aya za Qur'ani Tukufu, Hajja Hakima binti Muhammad Yusuf, mkuu wa kamati ya maandalizi aliwasilisha ripoti kuhusu kupangwa kwa mashindano hayo.

Alisoma majina ya wajumbe wa jopo la majaji na kuwashukuru wawakilishi wa nchi zilizoshiriki.

Waziri wa Masuala ya Kidini wa Malaysia Idris Ahmad pia alitoa hotuba ambapo alisisitiza kwamba Qur'ani Tukufu ni muujiza mkubwa ulioteremshwa kwa Mtukufu Mtume Muahmmad (SAW) na kwamba ni chanzo cha mwongozo na rehema kwa wanadamu wote.

Kisha, washindi wakuu wa mashindano ya mwaka huu  walitangazwa.

Bahraini Qari Wins Malaysia Int’l Quran Contest, Host Country’s Contender Comes 1st in Women’s Category

Kwa mujibu wa uamuzi wa jopo la majaji, Mohamed Sameer Mohamed Magahed, msomaji wa Qur'ani anayewakilisha Bahrain, alishinda mashindano ya mwaka huu katika kitengo cha wanaume. Alipata pointi 93.33 kati ya 100.

Qari ya Malaysia alikuwa mshindi wa pili na wale kutoka Indonesia, Iraq na Singapore waliibuka wa tatu hadi wa tano, mtawalia.

Katika kitengo cha wanawake, msomaji wa Malaysia Sofizah Mousin alitajwa kuwa mshindi wa juu, alipata 89.66.

Washindi wa daraja la pili hadi la tano walikuwa wawakilishi wa kike wa Singapore, Indonesia, Brunei, na Afghanistan.

Kwa mujibu wa habari,mshindi mkuu wa shindano hilo atarudisha MYR 4,000 pamoja na baa ya dhahabu yenye thamani ya MYR 40,000 hadi 50,000.

Bahraini Qari Wins Malaysia Int’l Quran Contest, Host Country’s Contender Comes 1st in Women’s Category

Duru ya mwisho ya toleo la 62 la mashindano ya kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Malaysia, inayojulikana rasmi kama Makusanyiko ya Kimataifa ya Kuhifadhi Qur'ani ya Malaysia (MTHQA), ilianza katika ukumbi wa KLCC siku ya Jumatano.

3480986

captcha