Supamaketi ya Souq Al Baladi imetangaza kuwa matawi yake yote hayatauza tena bidhaa zozote za Uswidi.
Klipu za video katika mitandao yakikamii zimeoonyesha wafanyakazi wakiondoa chokoleti maarufu ya Uswidi kwenye rafu. Ususiaji huo umekuja huku ulimwengu wa Kiislamu ukiendelea kulaani vitendo vya hivi karibuni vya kuvunjia heshima Qur'ani Tukufu nchini Uswidi.
Kitabu hicho kitakatifu kilichomwa au kuharibiwa wakati wa maandamano ya hivi karibuni ya umma katika mji mkuu wa Uswidi, na kusababisha hasira kote ulimwenguni.
Kukata uhusiano wa kisiasa na kibiashara kati ya nchi za Kiislamu na Uswidi sambamba kususia bidhaa za nchi hiyo pia inaweza kuwa sehemu ya kampeni kubwa ya Waislamu ya kupinga hatua ya serikali ya Uswidi ya kutoa kibali cha kuchomwa moto Qur'ani Tukufu nchini humo.
3484500